Higher Education Students' Loans Board

  • Dar es Salaam, Tanzania. P.O.Box 76068

  • General call +255 22 286 4643

  • Monday - Friday8:00am - 5:00pm

News & Events


31
August 2024

KUONGEZWA KWA MUDA WA MAOMBI YA MIKOPO 2024/2025

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu inapenda kuwafahamisha Waombaji wa mikopo na Umma kwa ujumla kuwa muda wa kuwasilisha maombi ya mikopo umeongezwa mbele hadi tarehe 14 Septemba, 2024.

Hatua hii imechukuliwa ili kuwapa fursa wale ambao kwa sababu mbalimbali hawakuweza kufanya maombi ya mikopo katika muda uliokuwa umepangwa.

Itakumbukwa kuwa, awali Bodi ilianza kupokea maombi ya mikopo kwa njia ya mtandao tarehe 1 Juni, 2024 na mwisho wa kuwasilisha maombi ulipangwa kuwa tarehe 31 Agosti, 2024.

Kupitia tangazo hili, waombaji wa mikopo kwa mwaka wa masomo 2024/2025 ambao hawajakamilisha maombi yao wanashauriwa kukamilisha na kuwasilisha maombi yao ya mikopo ndani ya muda ulioongezwa.

Bodi inapenda kusisitiza kuwa hakutakuwa na muda mwingine wa nyongeza baada ya tarehe 14 Septemba, 2024.

 

IMETOLEWA NA:

BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

Jumamosi, Agosti 31, 2024